Tuesday, December 22, 2009

T-SHIRT SAMPLE

Wadau, hii ni sample ya T-shirt ambazo tumekuwa tukizizungumzia sana! Tutatumia utaratibu wa order kupata T-shirt hizi. T-shirt moja ni 350 Rs. Kwa wote tutakaopenda T-shirt hizi, tutalazimika kutoa order hili T-shirt ziwe printed. Kwa maelezo zaidi, tuwasiliane kupitia 9840123784!

AD!!!

Tuesday, November 3, 2009

9 TANZANIAN STUDENTS ARRESTED IN MYSORE

10 foreign students arrested in city

Staff Correspondent
01 November 2009 THE HINDU
MYSORE: The Kuvempunagar Police on Saturday arrested 10 foreign students on the charges of assaulting three police constables and causing public nuisance.

Nine of the arrested are from Tanzania and the other one is a Kenyan national. Seven of them are studying in the JSS Law College and the rest in the SBRR Mahajana’s College, the police said.

Residents of Kanakadasanagar had complained to the police that the students were causing nuisance in the locality allegedly in an inebriated condition.

Around 4 a.m., three police constables went to the building in which the students were residing for an inquiry. However, the students assaulted them and tore their uniform, Kuvempunagar inspector Dhananjay said.

On learning about the incident, a police team led by sub-inspector Prasanna Kumar rushed to the spot and took the students into custody. Seven cars, two motorcycles and liquor bottles were seized, the police said.

Wednesday, October 28, 2009

NEW DESIGNS...

Hello, here's the new design, I hope you all like it! One has a white background, the other a gray one.. Please leave your comments!

Tuesday, September 1, 2009

TSHIRT IDEAS

TSHIRT IDEAS

Hello all, here are the tshirt ideas we've had so far. The first one was the initial idea, and after review by the Executive Council, it was decided we add a few details, which resulted with the final design. Clicking on it will give you a bigger picture! Please leave your comments!!!!!

INITIAL IDEA

FINAL IDEA!!!

Saturday, June 13, 2009

HAPPY BIRTHDAY WADAU

The Family of Tanzanians in Tamil Nadu are honored to celebrate this occasion with you Mr. Juma Kipande and Mr. Deogratius Mtui HAPPY BELATED BIRTHDAY AND MANY HAPPY RETURNS!

Monday, June 8, 2009

HAPPY BELATED BIRTHDAY JONATHAN


The Family of Tanzanians in Tamil Nadu are honored to celebrate this occasion with you Mr. Jonathan Seni HAPPY BELATED BIRTHDAY AND MANY HAPPY RETURNS!

Wednesday, May 27, 2009

HAPPY BIRTHDAY ALFRED P. MCHAU


You've left Tamil Nadu, but the community still recognizes your contribution to its formation! With this I'd like to wish you a HAPPY BIRTHDAY... THE COMMUNITY WISHES YOU A HAPPY YEAR AHEAD AND WISHES YOU ALL THE BEST AS YOU JOIN THE WORK-FORCE!

CONTEST!

Tanzanians in Tamil Nadu, heard of the Contest??? Well, we saw it a nice idea to have tshirts... Tshirts that'll let everyone know that we're Tanzanians, and show them where exactly Tanzania is, and show that we're proud to be Tanzanians...

All the gurus of Photoshop, Corel Draw, Illustrator... etc.. even free hand, as long as you can scan your designs... Send it to us thru our email... watanzania.tamilnadu@yahoo.com

Of course, what's a contest without a price... The winner shall be awarded....

We're waiting for the Ideas........!!!

Director of Communication - TACTN


Monday, May 18, 2009

APOLOGY

The Office of Communication and Registration of the TACTN apologizes for failing to acknowledge the birthdays of the following members in due time. Nonetheless, as customary, the Community was happy to celebrate the birthdays of the members, either present physically at the occasion or not!

Gloria Mark Njiu (02/05/2009)
Amonson and Awson Asseri (05/05/2009)
Brandy Revocatus (07/05/2009)
Zakaria Moshi (13/05/2009)

The Community Wishes You a Happy and Prosperous Year

Friday, April 24, 2009

HAPPY BELATED BIRTHDAY

The Family of Tanzanians in Tamil Nadu are honored to celebrate this occasion with you Mr. Terence Vusile Silonda. HAPPY BELATED BIRTHDAY AND MANY HAPPY RETURNS!

Monday, April 20, 2009

COMMENTS ENABLED

For quite sometime it hasn't been possible to leave your comments. Now you can leave your comments on any posted item on the blog... Feel free! Ila tuwe wastaarabu.

SHARE THE FUN

Is it your birthday? Did you see something interesting? Want to share some info? Well, what are you waiting for

You can send to us your pics and articles that you want to share with the rest of the Tanzanians in the Community. Anyone is eligible, be it from Trichy, Madurai, Ooty, Erode, Chennai, Salem or Coimbatore. Just drop us an email at: watanzania.tamilnadu@yahoo.com and leave the rest to us.


Director of Information, Communication and Registration
Tanzanian Community in Tamil Nadu

GODFREY ROCKY ASHEREHEKEA SIKUKUU YAKE YA KUZALIWA NA MARAFIKI ZAKE

Mdau Godfrey Rocky (aliyevaa kofia), mdau Aaron na rafiki yao wakiwa katika shughuli ya kumpongeza Rocky aliyesherehekea sikukuu yake ya kuzaliwa tarehe 17/4/09
Rocky akipongezwa
Wadau wa karibu wa Bw. Rocky wakipata chakula cha jioni pamoja katika shughuli ya kumpongeza Rocky.

Friday, April 17, 2009

The Family of Tanzanians in Tamil Nadu are honored to celebrate this occasion with you Mr. Godfrey Rocky. HAPPY BIRTHDAY AND MANY HAPPY RETURNS!

Thursday, April 16, 2009

Something to ponder about: You Are Being Lied to About Pirates

Who imagined that in 2009, the world's governments would be declaring a new War on Pirates? As you read this, the British Royal Navy - backed by the ships of more than two dozen nations, from the US to China - is sailing into Somalian waters to take on men we still picture as parrot-on-the-shoulder pantomime villains. They will soon be fighting Somalian ships and even chasing the pirates onto land, into one of the most broken countries on earth. But behind the arrr-me-hearties oddness of this tale, there is an untold scandal. The people our governments are labeling as "one of the great menace of our times" have an extraordinary story to tell -- and some justice on their side.

Pirates have never been quite who we think they are. In the "golden age of piracy" - from 1650 to 1730 - the idea of the pirate as the senseless, savage thief that lingers today was created by the British government in a great propaganda-heave. Many ordinary people believed it was false: pirates were often rescued from the gallows by supportive crowds. Why? What did they see that we can't? In his book Villains of All nations, the historian Marcus Rediker pores through the evidence to find out. If you became a merchant or navy sailor then - plucked from the docks of London's East End, young and hungry - you ended up in a floating wooden Hell. You worked all hours on a cramped, half-starved ship, and if you slacked off for a second, the all-powerful captain would whip you with the Cat O' Nine Tails. If you slacked consistently, you could be thrown overboard. And at the end of months or years of this, you were often cheated of your wages.

Pirates were the first people to rebel against this world. They mutinied against their tyrannical captains - and created a different way of working on the seas. Once they had a ship, the pirates elected their captains, and made all their decisions collectively. They shared their bounty out in what Rediker calls "one of the most egalitarian plans for the disposition of resources to be found anywhere in the eighteenth century." They even took in escaped African slaves and lived with them as equals. The pirates showed "quite clearly - and subversively - that ships did not have to be run in the brutal and oppressive ways of the merchant service and the Royal navy." This is why they were popular, despite being unproductive thieves.

The words of one pirate from that lost age - a young British man called William Scott - should echo into this new age of piracy. Just before he was hanged in Charleston, South Carolina, he said: "What I did was to keep me from perishing. I was forced to go a-pirating to live." In 1991, the government of Somalia - in the Horn of Africa - collapsed. Its nine million people have been teetering on starvation ever since - and many of the ugliest forces in the Western world have seen this as a great opportunity to steal the country's food supply and dump our nuclear waste in their seas.

Yes: nuclear waste. As soon as the government was gone, mysterious European ships started appearing off the coast of Somalia, dumping vast barrels into the ocean. The coastal population began to sicken. At first they suffered strange rashes, nausea and malformed babies. Then, after the 2005 tsunami, hundreds of the dumped and leaking barrels washed up on shore. People began to suffer from radiation sickness, and more than 300 died. Ahmedou Ould-Abdallah, the UN envoy to Somalia, tells me: "Somebody is dumping nuclear material here. There is also lead, and heavy metals such as cadmium and mercury - you name it." Much of it can be traced back to European hospitals and factories, who seem to be passing it on to the Italian mafia to "dispose" of cheaply. When I asked Ould-Abdallah what European governments were doing about it, he said with a sigh: "Nothing. There has been no clean-up, no compensation, and no prevention."

At the same time, other European ships have been looting Somalia's seas of their greatest resource: seafood. We have destroyed our own fish-stocks by over-exploitation - and now we have moved on to theirs. More than $300m worth of tuna, shrimp, lobster and other sea-life is being stolen every year by vast trawlers illegally sailing into Somalia's unprotected seas. The local fishermen have suddenly lost their livelihoods, and they are starving. Mohammed Hussein, a fisherman in the town of Marka 100km south of Mogadishu, told Reuters: "If nothing is done, there soon won't be much fish left in our coastal waters."

This is the context in which the men we are calling "pirates" have emerged. Everyone agrees they were ordinary Somalian fishermen who at first took speedboats to try to dissuade the dumpers and trawlers, or at least wage a 'tax' on them. They call themselves the Volunteer Coastguard of Somalia - and it's not hard to see why. In a surreal telephone interview, one of the pirate leaders, Sugule Ali, said their motive was "to stop illegal fishing and dumping in our waters... We don't consider ourselves sea bandits. We consider sea bandits [to be] those who illegally fish and dump in our seas and dump waste in our seas and carry weapons in our seas." William Scott would understand those words.

No, this doesn't make hostage-taking justifiable, and yes, some are clearly just gangsters - especially those who have held up World Food Programme supplies. But the "pirates" have the overwhelming support of the local population for a reason. The independent Somalian news-site WardherNews conducted the best research we have into what ordinary Somalis are thinking - and it found 70 percent "strongly supported the piracy as a form of national defence of the country's territorial waters." During the revolutionary war in America, George Washington and America's founding fathers paid pirates to protect America's territorial waters, because they had no navy or coastguard of their own. Most Americans supported them. Is this so different?

Did we expect starving Somalians to stand passively on their beaches, paddling in our nuclear waste, and watch us snatch their fish to eat in restaurants in London and Paris and Rome? We didn't act on those crimes - but when some of the fishermen responded by disrupting the transit-corridor for 20 percent of the world's oil supply, we begin to shriek about "evil." If we really want to deal with piracy, we need to stop its root cause - our crimes - before we send in the gun-boats to root out Somalia's criminals.

The story of the 2009 war on piracy was best summarised by another pirate, who lived and died in the fourth century BC. He was captured and brought to Alexander the Great, who demanded to know "what he meant by keeping possession of the sea." The pirate smiled, and responded: "What you mean by seizing the whole earth; but because I do it with a petty ship, I am called a robber, while you, who do it with a great fleet, are called emperor." Once again, our great imperial fleets sail in today - but who is the robber?

Saturday, April 11, 2009

SALAAM ZA PASAKA

Ndugu watanzania wenzangu, Nachukua nafasi hii kuwatakieni nyote kheri na fanaka tele za sikukuu hii ya pasaka. Naamini Pasaka kama zinavoweza kuwa sikukuu nyingine zozote za kidini inatupa nafasi muhimu ya kutuunganisha sisi watanzania na kujumuika.

Naomba kuwaalika nyote kutumia nafasi hii muhimu kukuza ushirikiano baina yetu watanzania bila kujali dini zetu. Kama ambavyo tungeweza kuunganika wote kwenye tafrija ya kusherekea Eid el Hajj  basi vivo hivo tutumie nafasi hii kama watanzani kwenye miji yetu kukusanyika na kujumuika. Nawasihi kuendelea kuukuza moyo wa ushirikiano tulionuia kuujenga kupitia jumuiya yetu.

Naamini wote kwa namna moja au nyingine tutapata furssa ya kusherekea sikukuu hii. Tukumbuke basi kuwashirikisha watanzania wenzetu katika kuadhimisha sikukuu hii.

Naomba tukumbuke vile vile kubadilishana picha za tafrija tutakazofanya kwenye miji yetu katika kuadhimisha sikukuu hii ili iwe chahcu katika kuhamasishana.

Nawatakia nyote pasaka njema.

Mwenyekiti,
Jumuiya ya Watanzania Tamil Nadu.

Friday, April 10, 2009

KIKAO CHA BARAZA LA JUMUIYA YA WATANZANIA TAMIL NADU





Mnamo tarehe 4 April 2009. Viongozi wa jumuiya ya watanzania Tamil Nadu wakiwemo viongozi wa kamati tendaji na wawakilishi wa matawi ya jumuiya kutoka miji husika walikutana mjini Tirruchchirapalli (Trichy) kwa ajili ya kikao cha kwanza cha ngazi ya baraza kama ilivyoainishwa kwenye katiba ya jumuiya.

Kikao hicho kilihudhuriwa na viongozi wa kamati tendaji pamoja na viongozi wa miji ya Trichy (wenyeji), Madurai na Chennai. Kikao hiko pia kilihudhuriwa na waalikwa kutoka miji ya Ooty na Erode kwa ajili ya kuja kujifunza na kubadilishana mawazo na uzoefu.

Miongoni mwa mambo yaliyaojadiliwa ni vipaumbele katika utendaji wa jumuiya kwa kipindi cha mwaka 2009, namna ya kuwahamasisha watanzania wa miji mingine kujiunga na jumuiya na taratibu za kiutendaji za baraza la jumuiya.

Akifungua kikao hicho Mwenyekiti wa Jumuiya ya Watanzania Tamil Nadu Ndg. Deus Valentine Rweyemamu aliainisha kuwa wakati wa kuandaa Kongamano la watanzania Tamil Nadu kipaumbele kilikuwa ni kuwakusanya watanzania waliopo Tamil Nadu. "Wakati wa kongamano tulijikita kujadili ni namna gani tutautunza na pale inapowezekana kuupanua mkusanyiko wetu, na ndipo wazo la kuunda jumuiya lilipoanzia kwahiyo tukaridhia na kupitisha katiba ili tuwe na chombo rasmi cha kutukusanya sisi kama Watanzania tunaoishi katika jimbo hili la Tamil Nadu."

Wajumbe walikubaliana kimsingi kwamba Jumuiya hii si chombo cha kisiasa ila ni utaratibu wa kurahisisha mahusiano ya kijamii kwa watanzania waliopo Tamil Nadu. Jumuiya itakuwa imefanikisha malengo yake kama mwisho wa siku itapelekea watanzania wa Tamil Nadu kujumuika zaidi, kufahamiana zaidi na kushirikiana zaidi.

Kulingana na Katiba ya jumuiya ya Watanzania Tamil Nadu kama ilivopitishwa Tarehe 26 Disemba 2009 Baraza la Jumuiya ni chombo cha maamuzi kinachoundwa na kamati tendaji na wawakilishi wa kila tawi. Baraza hili husimamia utendaji wa Kamati tendaji na ni chombo kinachotumika kuyashirikisha matawi yote katika kufanya maamuzi na hivyo kuwa na dau sawa (equal stake) katika uendeshaji wa jumuiya. Baraza hili kulingana na Kaitba hukutana kila baada ya miezi mitatu.

Tunatarajia kuwashirikisha habari zaidi punde tutakapopata miniti za kikao hicho kutoka kwa ofisi ya Katibu mkuu pamoja na tamko la baraza lilitokana na kikao hicho.

Tunawashukuru sana washiriki wa kikao kwa moyo wao wa dhati wa kujitolea. Wajumbe walikuwa tayari kujighramia kuhudhuria kikao hichi kwa moyo mkunjufu wakielewa wazi kuwa Jumuiya bado ni changa na haina uwezo wa kujiendesha ipasavyo kwa sasa. Tunawashukuru sana wenyeji wetu Trichy kwa kujitolea muda wao na kwa kuwa tayari kuchangia sehemu ya gharama za kikao.

Tunawashukuru vile vile dada zetu wa Madurai kwa kukubali kuwa wenyeji wa kikao kijacho cha baraza.

Kwa mawasiliano zaidi kuhusu kikao hichi pamoja na Ajenda zake wasiliana na Idara ya Habari, Mawasiliano na Uhusiano kupitia watanzania.tamilnadu@yahoo.com.

Mungu ibariki Tanzania, Mungu ibariki Afrika, Mungu awabariki nyote.

Aluta Continua!!!

Imetolewa  na Idara ya Habari, Mawasiliano na Uhusiano.
Jumuiya ya Watanzania Tamil Nadu.

Thursday, April 2, 2009

THE EXECUTIVE COUNCIL TO MEET IN TRICHY - 4/4/09

The first executive council meeting is expected to take place at Tirruchchirappalli on Saturday the 4th of April 2009. Delegates from Chennai, Erode, Madurai, Ooty and Trichy (the hosts), will be meeting with the Executive Committee to discuss the various issues regarding the Community. 

This being the first executive council meeting, it is expected to provide a very important opportunity for the members of the community to participate actively through their representatives/leaders in determining not only what they want the community to do for them but also what they want to do for the community. 

Among the issues to be discussed include the Action Plan for the year 2009, the Budget for the year 2009, the Restoration of new branches and many more. 

Stay tuned for the the proceedings and the resolutions of the First Executive Council Meeting.


Tuesday, March 31, 2009

MAPINDUZI TANZANIA

Katika mazingira ya kutatanisha yametokea mapinduzi ya kijeshi nchini Tanzania katika kipindi ambacho nchi nyingine zaidi ya tano barani Afrika(Mauritius,Equotorial Guinea, Madagascar,Ghana&Comoro)zimepitia mapinduzi kama hayo ya kijeshi.

Majira ya saa 3 na nusu wanajeshi wanaosemekana kutoka kambi ya anga ya Ngerengere na kikosi ya Nyumbu, Msangani walivamia eneo la ikulu jijini Dar es Salaam ambapo Rais Jakaya Kikwete alitegemewa kuwa na Hafla kwa heshima ya Muwakilishi wa Malkia wa Uingereza Gavana Quentin Bryce wa Australia

Wanajeshi hao wanasemekana kupanga njama za kuzima umeme wa eneo zima la ocean road na feri ambapo ofisi muhimu za serikali zipo. Mpaka hivi sasa haijafahamika kama wafanyakazi wa shirika la umeme nchini TANESCO walihusika kwenye njama hizo.

Mpaka tunaingia mitamboni haijafahamika Rais Kikwete yuko wapi kwani wanajeshi hao waasi hawajathibitisha kumtia nguvuni. Hata hivo inasadikika Rais alipata nafasi ya kutoroka kama ilivyokuwa katika mapinduzi ya mwaka 1964 ambapo baba wa taifa alifanikiwa kuwaponyoka waasi walipovamia ikulu.

Wadadisi wa mambo ya kisiasa wametoa maoni yao kuhusu tukio hili huku wengi wao wakisisitiza kuwa sio jambo la ajabu sana kwani wimbi la mapinduzi limeonekana kuliteka bara la Afrika katika kipindi cha mwezi mmoja uliopita. Kulingana na maelezo yao inawezekana wanajeshi wa Tanzania wameamua kuiga mfano wa wenzao waliotangulia na inawezekana mapinduzi haya yakaendelea katika nchi zingine. Imethibitika kuwa hali ngumu za kiuchumi, kupanda mno kwa gharama za maisha na kushuka kwa maadili katika jamii ndio vimekuwa vichocheo vikubwa katika bara la Afrika kwa kipindi hiki.


Wakati ukisoma habari hii kumbuka leo ni siku ya wajinga duniani na WAJINGA NDIO WALIWAO. 

Monday, March 30, 2009

Sunday, March 29, 2009

Ajali Dar: Chenge adaiwa kujuana na mmoja wa marehemu
Waziri wa zamani wa Miundo Mbinu na Mwanasheria Mkuu, Andrew Chenge ambaye gari lake liligongana na Bajaj na kuua wanaweke wawili mmoja wao akifahamika kuwa anajuana naye.


 

SAKATA la ajali ya gari la Andrew Chenge ambalo limesababisha vifo vya wanawake wawili, limeingia katika sura mpya baada ya ndugu wa wasichana hao kudai kuwa Chenge alikuwa akimfahamu mmoja wa marehemu.

Chenge ambaye alikuwa Waziri na Mwanasheria mkuu wa zamani wa serikali, aliingia matatani baada ya gari alilokuwa akiendesha kugonga "bajaji" usiku wa kuamkia juzi na kuua wanawake wawili ambao ni Beatrice Costantine ambaye ni mfanyabiashara wa Mwanza na mmiliki wa saluni ya kike na Vicky George Makanya.

   

Wakizungumza kwa nyakati tofauti jijini Mwanza baadhi ya ndugu waliohojiwa na Mwananchi Jumapili akiwamo mama mzazi wa Vicky, walisema wanafahamu Chenge kuwa alikuwa akimjua ndugu yao Vicky.

Akizungumza na Mama wa marehemu Vicky, Nazifa Kambi nyumbani kwao Iloganzala ambako kuna matanga alisema amesikitishwa na taarifa za upotoshaji zilizoeleza kuwa mwanae na rafiki yake walikuwa wakienda Zanzibar kwa ajili ya kufunga ndoa jambo ambalo alilipinga na kueleza kuwa alikuwa akija Mwanza baada ya kutoka Zanzibar ambako walikwenda kununua vifaa vya saluni ya mwenzake.

          “Ajali hii inanipa mashaka makubwa kutokana na kupokea taarifa za kupotosha za kufunga ndoa," alisema.

Alisema pia amepata taarifa kutoka kwa wafanyakazi wenzake kuwa Chenge walikuwa wakifahamiana na Vicky na kwamba kila mara alipokuwa akifika Mwanza Hotel alikuwa akimtaka kumhudumia vinywaji yeye.

      Nazifa alisema marehemu Vicky ambaye alikuwa mfanyakazi wa Mwanza Hotel katika kitengo cha King Casino ambayo kwa sasa inajulikana kama The Stone, hata yeye mwenyewe aliwahi kumsikia mwanaye kuhusu mbunge huyo kumtaka atoke nyumbani kwenda kumhudumia siku ambayo hakuwa kazini.

Ameiomba serikali kufanya uchunguzi wa kina kuhusu ajali hiyo ili kupata nini kilichosababisha ajali hiyo.

Kwa upande wa msemaji wa familia ya Beatrice, kaka wa marehemu, Andrew Costantine akiwa Kiseke kwenye matanga alisema wanachofahamu wao ni kuwa dada yake amepatwa ajali akiwa njiani kurejea hotelini walikofikia ya JVL Hotel iliyopo Mwananyamala wakati wakitoka Oysterbay kwa ajili ya kuchukua mizigo yao tayari kwa kuondoka Dar es Salaam kwenda Mwanza.

Andrew alieleza kuwa tayari marehemu na rafiki yake walikuwa wamekwisha kutoka Zanzibar ambako walikwenda kununua bidhaa na vifaa vya saluni ya kike ambavyo vimekutwa hotelini walikokuwa wamefikia.

Alisema marehemu hakuwa amekwenda kufunga ndoa Zanzibar kwa vile alikuwa na mume wake ambaye ni mzungu raia wa Marekani na kwamba mpaka anafikwa na mauti mme wake alikuwa nje ya nchi.

Alisema habari zilizotolewa na baadhi ya vyombo vya habari kuwa walikuwa wakienda kufunga ndoa siyo za kweli.

“Wakati wakiondoka alimuaga rafiki yake Khadija Hassani ambaye ndiye alimuachia nyumba yake na wakati akiwa Zanzibar alimtumia fedha kwa ajili ya kuwalipia ada ya shule watoto, sasa mambo mengine hakuna anayejua tunaomba uvumulivu msiba uishe,” alieleza.

Alisema mpaka sasa Chenge ameahidi kusaidia familia kusafirisha miili ya marehemu hao, lakini bado hawajapokea lolote kutoka kwake na wanaendelea kumsubiria wakati polisi wakikamilisha taratibu za uchunguzi huku na wao wakijipanga kusafirisha miili ya ndugu zao.

Msiba hii imeacha simanzi Jijini Mwanza na kuwa gumzo kubwa huku ukizua minog’ono ya hapa na pale na baadhi ya wakazi wa jiji la Mwanza wengine wakishangazwa na tukio hilo na jinsi jeshi la polisi lilivyounda tume kushughulikia ajali hiyo tofauti na ajali nyingine.

Marehemu hao waliondoka Jijini Mwanza Machi 24, mwaka huu kwa safari ya kibiashara Dar es salaam na baadaye Zanzibar na walikuwa wakitarajiwa kureja Ijumaa Machi 27, Beatrice ameacha watoto wanne ambao wanasoma shule tofauti za bweni na mwenzake Vicky ameacha mtoto mmoja mwenye umri wa miaka mitano.

Hata hivyo, juhudi za kumpata Chege kwa simu jana hazikuzaa matunda jana.

UMESHASIKIA KUHUSU RICHMOND ILIYOMFUKUZISHA KAZI LOWASA

“Giza Nene”?
Mwishoni mwa mwaka jana, gazeti moja nchini liliandika habari zenye kichwa, “Giza Nene” kuhusu sakata la kampuni moja “bandia” ya Amerika ya kufua umeme wa dharura nchini Tanzania. Wote tunaijua kampuni hii. Na mmojawapo wa wakurugenzi wake, Naeem Mohamme, sasa kafikishwa mahakamani kwa tuhuma za kusema uwongo na ufisadi!
Wengi wetu bado tumo katika “giza nene” la sakata la Richmond kwa kutoelewa tunazungumzia kampuni zipi! Sijui ni makosa ya vyombo vya habari. Tusomapo au tusikilizapo habari kuhusu sakata hili, yaonekana kuwa kuna kampuni sita zinazotajwa tajwa (mbali na kampuni mbili za Dowans (Afrika Kusini na Tanzania):
Richmond Development Co. (RDC); Richmond Development Corporation (RDEVCO); Richmond Development, LLC.; LLC.; Richmond Tanzania Limited; na Richmond Development (Tanzania), Ltd.
Kwahiyo, kabla ya kuelewa “giza nene” lililotangazwa na gazeti hilo, ingekuwa vizuri tusaidiane kuliondoa. Tubakie na kampuni mbili za awali. Nionavyo, kuna kampuni mbili tu. Moja, ni kampuni tanzu ya utata ya Richmond Development Company of Houston (RDEVCO) iliyojidai kusajiliwa huko Houston, Texas, na kampuni-toto ya Richmond Development Company Tanzania, Ltd. iliyosajiliwa nchini Tanzania, pia kwa utata. Wakati mwingine yaandikwa kama Richmond Development Company (Tanzania), Ltd. Hii ina maana kuwa ni “extension” ya kampuni tanzu ya huko Houston!
Kampuni iliyosajiliwa huko Houston, Amerika, ilijulikana kwanza kama Richmond Development Corporation (RDC). Lakini sasa yajulikana kama Richmond Development Company of Houston (RDEVCO). Kampuni hii iliundwa na mmoja wa familia ya Gire ya huko Houston, Mohamed S. Gire. Hao akina Gire ni Wahindi wa kutokea Tanzania!
Akina Gire hao Bwana Mohamed S. Gire (Alim Gire) wana kampuni ya ki-familia yenye kuchapisha na kurudufu “nyaraka” ijulikanayo kwa jina la Richmond Printing Company. Bwana Mohamed S. Gire (Alim Gire) ni Chief Executive Officer). Wengine ni ndugu zake: Samad Gire (Vice President, Business Development), Javeed Gire (Manager), Zahoor Gire (Vice President Finance), na Imad Gire (Vice President Operations). Dada zao wawili wanaishi nchini Uingereza, ambako baba yao alikwenda kuishi, kama mfanyabiashara. Anwani: Richmond Printing L.L.C. ni 5825 Schumacher Lane, Houston, Texas 77057.
Kampuni zote mbili, Richmond Printing Company na Richmond Development Company of Houston (RDEVCO), zinatumia fax moja: (713) 952-0932-5825. Hii ina maana kuwa kampuni hizi mbili zinatumia, pengine, jengo moja.
Tovuti ya mwanzo ya Richmond Development Corporation ilionyesha historia ya habari za Gire kuhama Chicago kwenda Houston kuanzisha kampuni ya kurudufu nyaraka (“copying centre”) iitwayo, Richmond Printing Company, mwaka 1985. Pia kulikuwa na habari nyingi za michango ya Bwana Mohamed S. Gire ya takrima na kutunisha mfuko wa kampeni za Democratic Party (“political campaigns contributions”) kwa House of Representatives.
Inaonekana kuwa Richmond Development Corporation (RDC) ilibadili jina na kuitwa Richmond Development Company (RDEVCO). Lakini sasa vyombo vya habari vinaitaja kama Richmond Development, LLC. Na mara nyingine inatajwa tu kama LLC.
Je, Richmond Development Corporation (RDC) au Richmond Development Company (RDEVCO au LLC ilijuaje kuwepo kwa makaribisho ya zabuni za kufua umeme wa dharura na hali wako huko Texas, Amerika? Nafikiri kuwa huyo Mohamed Gire wa Marekani alipata kujua uhondo wa tenda hiyo kutokana na “dugu” yake Naeem Gire wa Dar es Salaam!
Alichofanya Mohamed Gire ni kuunda kampuni uchwara ya Richmond Development Corporation (RDC) na kumkaribisha mtu mwingine aliyebobea katika utalaamu wa ki-biashara, Dr. Mohammed S. Huque, (mwana-uchumi m- Pakistani/m-Amerika), ambaye ni Mkurugenzi-Mwenza.
Na kuna habari za kuaminika kuwa hao akina Gire (Mohamed na Neem) na huyo Dr. Huque walikuwamo katika tenda nyingine yenye utata ya kujenga bomba la kusafirisha mafuta kutoka Dar es Salaam hadi Mwanza. Na hata tovuti yao iliwahi kuandika kuwa kati ya miradi iliyotekelzwa ni ujengaji wa bomba la mafuta katika mojawapo ya nchi zinazoeendelea.
Na kuna habari kwamba huyo Naeem wa Dar es Salaam, alikuwa pia na u-wakala wa kuuza majumba ya serikali! Ndio kusema kuwa yupo karibu karibu na baadhi ya “vigogo” na “wakubwa” wa serikali na chama chao tawala, CCM.
Kufuatana na mantiki hii, huyo Naeem Gire wa Dar es Salaam ndiye aliwaatarifu hao ndugu zake wa Houston, Texas, kuweko kwa tenda ya kufua umeme wa dharura, kutokana na ukame uliokithiri ufauji wa umeme kwa kutegemea maji ya mabwawa yetu.
Baada ya Richmond Development Company (RDC) kupewa hiyo tenda, huyo Naeem Gire wa Dar es Salaam alisajili upesi upesi kampuni nyingine ya Richmond Tanzania Limited au Richmond Development (Tanzania), Ltd. kwa ofisi ya Wakala wa Usajili wa Makampuni na Majina ya Biashara (Brela), “…Julai 13, 2006 ikiwa ni mwezi zaidi ya mmoja baada ya mkataba huo kusainiwa, ikiwa na wanahisa wawili ambao ni LLC na Naeem Gire.”
Cha kutatanisha ni kuwa Kampuni hii ya Richmond Development Company inabadilika badilika. Kama nilivyotaja hapo awali imebadilika na kupewa jina la Na sasa jina linalotumika ni la Richmond Development Company, LLC. Na hapo juu bwana Naeem Gire anakiri kuwa jina la kampuni ni “…LLC...”, kama alinukuliwa vizuri!
Ukweli ni kwamba Richmond Development Company au Richmond Development Company of Houston (RDEVCO) au LLC haina na wala haitengenezi hizo mashini za kufua umeme (turbines)! Ni kampuni ya u-wakala tut u chini ya Mohamed A. Gire (m-biashara Mhindi m-Tanzania/m-Amerika na Dr. Mohammed S. Huque, (mwana-uchumi m-Pakistani.m-Amerika).
LLC si jina la kampuni; ni kifupi cha maneno ya Kiingereza, “limited liability company”, sawa na neno tulilozea la “limited”, au kwa kifupi, “Ltd”! Kwahiyo, badala ya kuandika Richmond Development Corporation, Ltd. huandikwa Richmond Development Corporation (LLC)! Usajili wa kampuni ya LLC. au Ltd. ni uchu wa u-nyang’au Yutaka kunyonya kwa kujikinga ki-sheria endapo itafikishwa mahakamani kudaiwa! Au isihitajike ki-sheria kuwataja wenye hisa wake! Kama wenye hisa hizo ni “wakubwa na vigogo” wa Tanzania, twafa!
Katika hali ya utata, Richmond Development Company of Houston (RDEVCO), au kwa kifupi, RDEVCO, ilijitoa katika tenda hiyo ki-siri siri na kuirithisha kampuni ya Dowans. Tulielezwa kuwa kampuni hii ya Dowans ni ya mojwapo ya nchi za ki-Arabu huko Mashariki ya Kati!
Lakini sasa yajulikana kuwa Dowans Holdings SA ni ya huko Afrika Kusini! Baadaye, kama walivyofanya kuhusu Richmond Development Company Tanzania, Ltd. waliunda kampuni nyingine ya Dowans Tanzania, Ltd. Pengine, ni janja tu ya “danganya toto”; ni wale wale! Richmond Development Corporation (RDEVCO) = Dowans Holdings SA; na Richmond Tanzania, Ltd. = Dowans Tanzania, Ltd.
Sakata hilo limesababishwa na unyonge wa m-Tanzania katika kufua nguvu za umeme/nishati, kwa upande mmoja, na uchu wa u-nyang’au wa walalaheri, kwa upande mwingine, wanaokula njama na ma-wakalakuichoma na kuiangamiza nchi yetu kwa maslahi yao na watoto wao!
Kuna mengine yaliyofichwa na Tume ya Bunge, chini ya m-Bunge Harrison Mwakyembe (CCM-Kyela Magharibi). Na cha kushangaza ni kwamba TAKUKURU haikuona cha ufisadi katika sakata hili!
Awali kwenye tovuti yao “Richmond” waliandika kuwa miradi yao ni pamoja na kujenga bomba lenye urefu mkubwa la kusafirisha mafuta katika nchi moja inayoendelea. Nafikiri hili bomba ni ule mradi waliokuwa wameukania wa kujenga bomba la mafuta kutoka Dar es Salaam hadi Mwanza.
Lakini sasa maelezo hayo yamefutwa na badala yake wanajidai, In 2006, we completed the Ubungo Emergency Supply Power Plant Project in Dar es Salaam, Tanzania. We provided full project development and engineering, procurement and commissioning (EPC) for the first 25MW, and all preparatory work for the second phase, of a 100MW ISO gas-based generation plant.”
(Tafsiri yangu: Mwaka 2006 tulitekeleza Mradi wa Kufua Umeme wa Dharura wa Ubungo, Dar es Salaam, Tanzania. Tulikidhi yote ya mradi huo ikiwa ni pamoja na uhandisi, kununua na kuweka mashini za kufua umeme wa 25MW, na matayarisho ya awamu ya pili ya mitambo ya gesi yenye uwezo wa kufua umeme wa 100MW ISO.)
Katika ripoti ya Mwakyembe au ya TAKUKURU, hatukusikia mchakato wa Ofisi ya u-Balozi wa Tanzania nchini Amerika! Maafisa wa juu u-Balozi wetu huo waliandikwa wakisifiwa kutokana na utekelezaji wa sera mpya ya ki-balozi (“new economic diplomacy”) iliyokitangazwa na Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje na Uhusiano wa Kimataifa wa zamni, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete, wakati wa Awamu ya Tatu.
Balozi na Msaidizi Mkuu wake walijua (na wanajua wazi) matayarisho ya Mohamed A. Gire katika kufanikisha mkataba huo wenye utata. Bwana Mohamed A. Gire aliwakaribisha ma-Balozi wetu hao kumtembelea na kuzuru Houston, Texas! Si ajabu, pengine, aliwalipia nauli na mahali pa kulala hapo Houston!
Wa-Tanzania wa huko Houston wengi walifikiria kuwa Balozi na Msaidizi Mkuu wake walikwenda huko kuwatembelea wao! Soma taarifa ya habari zilizopokelewa na kuandikwa na ripota wa Guardian (ippmediaonline ya 2003-08-19 10:21:22). Sijui chanzo cha habari hii; pengine, kilikuwa ni sehemu ya Idara ya Habari na Utangazaji ya Ofisi ya Ubalozi wa Amerika nchini Tanzania, u-Balozi wee nchini Amerika au kutoka huko Houston, Texas.
Zaidi, habari zilizoandikwa na mojawapo la magazeti ya nyumbani, THISDAY, ziliwahi kueleza kwa undani na kuyataja majina ya walioshiriki katika tenda ya ufisadi wa Richmond wenye mtaji wa shilingi karibu milioni 173-!
Sakata la ufisadi wa Richmond, lilitangulia ujio wa Rais Bush wa Amerika, likiongezea kutonesha kidonda cha wa-Tanzania waliposikia kuwa kampuni ya Richmond Development Company (LLC) ikitamka kuwa iliingia mkataba na serikali ya Tanzania wenye thamani ya dola za ki-Amerika milioni 83. Lakini serikali ilitamka kuwa kondrati hiyo ilikuwa na thamani ya shilingi bilioni 172.9/-.
Richmond Development Company (LLC), ilikataa kata ikisema kuwa haijapokea na kwamba hakuna hata mfanyakazi wake hata mmoja amewahi kulipwa "ki-jisenti” kimoja kutoka serikali ya Tanzania au afisa wake ("a single penny from, or paid a penny to, the government of Tanzania or any of its officials.")
Wa-Tanzania walibaki wakijiuliza maswali mawili muhimu:
Moja, je, “sirikali” imekuwa ikimlipa nani kiasi cha dola za ki-Amerika 140,000 elfu, kila siku!
Mbili, kwa nini Richmond Development Company (LLC) haikusitisha mkataba endapo ilikuwa haijapokea malipo yeyote kutokana na kukamilisha kazi iliyopewa? Kwani kwenye tovuti yake, Richmond Development Company (LLC) inautangazia ulimwengu, kama nilivyonukuu kwa Kiingereza hapo juu, kazi iliyotakiwa kufanywa na kumalizika.
Huyo ndugu ya Mohamed A. Gire aliyeko Dar es Salaam (Naeem Mohamed) anajua zaidi makubaliano hayo ya ki-biashara! Na pai anawajua wenye hisa katika kampuni zote mbili. Ni lazima mahakama ikaze nati kwake!
Huenda, huyo Gire wa Dar es Salaam anao “insiders” wake katika Tanesco au/na Serikali! Huenda, huyo Naeem Gire wa Dar es Salaam yu karibu karibu na “vigogo” na “wakubwa” fulani wa serikali ya Tanzania na chama chao tawala ambao ni walikuwa ni wana-hisa katika Richmond Tanzania Ltd. au wenye hisa katika Dowans Tanzania Ltd!
Hao “vigogo” na “wakubwa” ndio waliomkaribisha Naeem Gire kuvua tenda! Labda, katika uchu wa u-nyang’au, waliunda kampuni ya siri siri, bila kuwataja rasmi wenye hisa katika kampuni hiyo ya Richmond Development Corporation (Tanzania), Ltd. Na hapo baadaye kwa siri kubwa wakaunda kampuni ya maficho (“offshore”) ya “ki-fisadi” na kuisajiri huko Mauritius ili wasilipe kodi kwa Tanzania au Afrika Kusini – kampuni ta Dowans!
Kuna wana-habari wengi ambao kwa muda mrefu wamekuwa wakiandika juu ya ufisadi na maingiliano ya siasa na biashara. Kuna misamiati mipya inayosimulia mwingiliano huo, “ubiasharishaji wa dola na usiasishaji wa biashara”.
Mwandishi Padre Karugendo wa RaiaMwema aliwahi kuandika akionya, “Michakato hii miwili, yaani ubiasharishaji wa dola na usiasishaji wa biashara inaendelea hapa Tanzania hivi sasa chini ya utawala wa CCM. Ni mfumo ambao umeshika kasi kiasi cha kutisha...”
Zaidi, Padre Karugendo, akiandika juu ya nia nzuri ya “(u)binafsishwaji wa mashirika ya umma”, Padri Karugendo alijutia sera hizo: “…wananchi hawakuelezwa bei za kuyauza mashirika hayo ambazo hazikufanana na bei za soko zililikuwapo wakati huo. Bei zilikuwa chini kwa kiwango kikubwa mno.”
Makala hiyo ya Padre Karugendo iliendelea kuelezea kile kinachowashangaza wengi. Aliandika:
“Baadhi ya kampuni zilizobinafsishwa zilinunuliwa na mawaziri na watumishi wa Serikali wa ngazi za juu kupitia makampuni yao au yale waliyokuwa wana hisa ndani yake. Maana yake ni kwamba bei zilipindwa ili kuwapendelea.
Zoezi hili liliwasaidia viongozi wa Serikali kupata mitaji. Watu hawa walikuwa na nyumba zao, na wengi wao wakawa wamesipangisha na kukaa katika nyumba za Serikali. Ukarabati uliofanyika kwenye nyumba hizi unaonyesha kwamba zinatumiwa kama dhamana ya mikopo, maana ziko katika maeneo yenye thamani ya juu.”
Je, pengine hiyo ndio sababu ya baadhi ya ma-Waziri na hata Rais wa Awamu ya Pili na ya Tatu kujiingiza katika mambo ya biashara! Kulikuwepo na mtindo wakati wa Awamu ya Tatu ya Rais Benjamin Mkapa kwa baadhi ya “vigogo” na “wakubwa” wa chama tawala na serikali yao kukamata vya umma shauri ya uchu wa u-nyang’au wao, ili usemi “Chukua Chako Mapema”, utimie hivi, mithili ya unabii!
Waziri wa Uchukuzi na Mawasiliano Ernest Nyanda (marehemu) wa Awamu ya Kwanza, Pili na Tatu alisemekana aliunda kampuni yake ya Victoria Marine Passenger Transport Services Ltd. na kukopa pesa za EPA kununua meli ya “mv Zahara”, ambayo utata wake, sijui, umeishia wapi!
Waziri Nizar Kamaragi naye kaunda kampuni ya “ukuli” (Tanzania International Container Terminal Services (TICTS), hapo bandarini, ambayo inazidi kuleta utata wa ki-upendeleo.
Naye aliyekuwa “amiri jeshi mkuu” wa wizara zote, Rais Benjamin Mkapa, mkewe pamoja na Waziri Yona walinunua kampuni ya umma kwa bei ya “karanga”! Ofisi ya kampuni yao ilikuwa hapo Ikulu. Si ajabu hiyo ofisi ilikuwa ndiyo “maktaba binafsi yake” iliyoungua kwa pasi wakati “amiri jeshi mkuu” akiwa safarini huko Masasi nje kabisa na hapo Ikulu!
Hivi hawa viongozi wa serikali wanapata wapi muda wa kuhudumia hizo kampuni zao binafsi na hali wakiwa bado wafanyakazi wa serikali! Pengine, ndio maana hawana muda wa kutosha wa u-nahodha wa “mitumbwi, meli na ndege zetu”. Sio viongozi wa serikali tu kuna, pia, viongozi wa chama tawala ambao ni ma-Waziri na wafanyabiashara binafsi!
Je, wanatumia wakati wa umma kujinufaisha? Je, wanalipwa mshahara kwa kufanya kazi za umma na huku wanatumia muda huo huo kushughulikia maslahi yao binafsi? Wakati wa Azimio la Arusha majambo haya hayakuwezekana!
Ilituweze kuondoka na “ubiasharishaji wa dola na usiasichaji wa biashara”, ambako kunaangusha taifa letu, mwandishi mwingine wa Raiamwema Ayubu Rioba aliwahi kushauri: “Tunahitaji fikra mbadala kutuwezesha kupunguza vifo vingi visivyo vya lazima katika nchi yetu; vifo vya kifikra (vinavyodhihirisha ujuha wetu katika mikataba mibovu, wizi wa BoT, Richmond, mtambo wa kuonea ndege, ndege ya rais, n.k.) na vile vya kimwili kama tunavyoendelea kuvishuhudia kwa majonzi kila kukicha.”
Kusema kweli waliotia saini mkataba huo ni kampuni ya Richmond Development Corporation (LLC) na Tanesco! Katika mikataba mingi kati ya Tanzania na wawekezaji wa nje kuna kifungu cha PSA (Production Sharing Agreement): Mfano, mwekezaji kubaliwa A anaweza kushirikiana na mwekezaji mwingine mpya chaguliwa B katika mkataba uliosainiwa na mwekezaji A, endapo ataiarifu na kupata idhini ya serikali ya Tanzania.
Ukiangalia makampuni yaliyokwishajiingiza katika mikataba mingi ya awali baina ya Tanzania na wawekezaji wa nchi za nje, utagundua msululu wa makapuni mapya ya PSA, kwa mfano, mikataba ya migodi ya madini na gesi. Ndio maana ingawa Rais Jakaya Kikwete aliamuru mikataba mingine mipya isisainiwe hadi hapo Tume ya Jaji Bomani itakapopitia na kutoa riporti yake kwa serikali. Bado tunayangoja hayo ya Utekelezaji wa Ripoti ya Jaji Bomani! Lkini kila mara mikataba ya PSA mipya inafunguliwa na kutiwa saini.
Ukiachilia mbali hayo ya Tume ya Jaji Bomani, si siri kwamba makampuni ya madini ya dhahabu na gesi yamekuwa yakiongeza wawekezaji wapya, kupitia PSA, na serikali ya Tanzania kuridhia makubaliano hayo bila kizuizi chochote.
Napenda sana PSA imulikwe wazi. Makampuni ya migodi ya dhahabu, almasi, nickel na uranium, na visima vya gesi na mafuta huingiza wawekezaji wapya kupitia PSA hususan pale ambapo serikali yetu huwapa hao wawekezaji kumiliki maliasili yetu kwa 100%! Inakuwa ni mali yao; na wanayo haki ya kuigawa mali hiyo kwa wale wawapendao. Kwani kila mara huwa ni wageni tu wanaoruhusiwa kutumia kipengere cha PSA! Pengine, wazawa nao huwa ni sehemu ya siri siri! Je, hii ni janja ya “vigogo” na “wakubwa” wa serikali na chama chao tawala kuweza kupata lolote kutokana na uhondo huo?
Nashauri kuwepo na u-wazi wa kuhusu si makampuni mapya yaliyojiingiza kupitia PSA bali pia uwazi wa kuhusu wazawa wapi walio na hisa katika makampuni hayo. Kwa nini nashauri hivyo? Mambo matatu ya wazi yanayozalisha “vi-ji-senti”.
Moja, ni utata wa kampuni ya Richmond Development Corporation (LLC), ambayo mambo yaliyojitokeza yalifunua shinikizo la “vigogo” na “wakubwa” wa serikali kukiuka ushauri wa wataalmu wa Shirika la Tanesco! Sio ajabu, “vigogo” na “wakubwa” wa serikali na chama chao tawala wana hisa katika Kampuni ya Richmond Development (Tanzania) Ltd! Na sasa kampuni hii inawalinda kwa kutolopoa ni akina nani wana hisa katika kampuni hii licha ya Naeem Gire!
Mbili, Mheshimiwa m-Bunge “kijana” Zitto Kabwe (CHADEMA Kigoma Rural) alikuja na tuhuma dhidi ya aliyekuwa Waziri wa Umeme na Nishati Nizar Karamagi kukimbia huko London hima na kusaini mkataba eti akiwa hotelini na kampuni ya migodi ya dhahabu ya Barrick huko Buzwagi! Pengine, Mheshimiwa Waziri wa Umeme na Nishati Nizar Karamagi alitia saini yake kuridhia tu mkataaba wa awali wa Barrick kwa kupitia mapatano ya PSA!
Tatu, aliyekuwa Waziri wa Umeme na Nishati Bwana Nizar Karamagi, huyo huyo, ana pia kampuni yake ya “ukuli” hapo Bandarini. Sijui naye aliiunda lini? Pengine, alijua kuwepo kwa PSA. Hivyo, kaiunda kampuni hiyo, ambayo hatuwajui wenye hisa, na hapo baadaye Rais Benjamin Mkapa kuiongezea muda wa kumiliki “ukuli” hapo bandarini kutoka miaka 15 hadi 25 bila kibali rasmi!
Tunaambiwa kuwa Tanzania iliingia mkataba na kampuni moja ya Houston, Texas, Amerika, ya Richmond Development Corporation, LLC. yenye kuzalisha au kufua umeme wa dharura kutokana na ukame uliosababisha mabwawa yetu ya maji kutosetri kuzalisha umeme. Wamiliki wa Richmond Development Corporation, LLC. Ndio walikuwa na 100% za hisa za kampuni hii.
Lakini cha kushangaza ni kwamba “wamiliki’ fulani walipoona uhondo upo katika mkataba huo, waliunda kampuni yao ya Kampuni ya Richmond Tanzania LTD na kuisajili “mwezi zaidi ya mmoja baada ya mkataba huo kusainiwa. Wana hisa wa kampuni hii ni LLC na Naeem Gire, kulingana na habari rasmi tupatazo, kama ifuatavyo: “(k)atika mchanganuo wa hisa, Gire ana miliki 250,000 na LLC 750,000 huku ikianza na mtaji wa Sh1,260,000,000 (1.2 bilioni).”
Je, si huyu huyu “mfanyabiashara” aliyeshindwa kabisa kuweza kupata mapesa ya kusafirishia mitumba yake hadi hapo serikali yetu ilipoingilia kupia Tanzanian Rural Development Bank (TRDB) – ambayo kwa bahati mbaya ofisi yake ya Barabara ya Lumumba iliungua moto!
Halafu kukaja ya Waziri “Vi-ji-senti”! Kauli ya Waziri wa Miundombinu Andrew Chenge (aliyejiuzulu) kuita dola za ki-Amerika milioni moja (pengine, hongo) anazotuhumiwa kuzificha Ulaya, kuwa ni “vi-ji-senti” ilitingisha muktadha wa lugha toka “semantics, pragmatics (logic)”, “linguistics” hadi “semiotics”! Waziri Chenge alieleweka! Waziri wetu huyu alipaka matope hali halisi ya walalahoi wa Tanzania! “Kiongozi” huyu alijikweza! Kiongozi huyu alikiuka kiapo chake!
Miktadha ya “diminutive or miniature” (kupunguza hadhi na thamani) katika lugha za Kisukuma, Kiswahili na Kiingereza si tofauti. Hivyo, ki-lugha Bwana Chenge alitupiga chenga za kuibia! Kimanufaa, kwetu komputa ya laptop ni komputa tu kama ile ya zamani iliyokitumia “punch card! Kimanufaa, kwetu kiselula ni simu tu sawa na zamani ya kuzungusha kwa mkono! Kimanufaa, kwetu sisi “vi-ji-senti” vipatavyo milioni moja (kwa dola za ki-Amerika) ni dola za ki-Amerika milioni moja hata kama Bwana Chenge ataziita “vi-ji-senti”!
Zaidi, Bwana Chenge mwanasheria wa vyuo vikuu vya Dar es Salaam (Tanzania) na Harvard (Amerika). Kwa kawaida, wana-sheria huwa makini sana katika matumizi na maana ya maneno! Bwana Chenge hakuiita hizo pesa zilizotajwa, “vi-senti”; aliziita, “vi-ji-senti”!
Na katufundisha kuwa kama hizo pesa ni “vi-ji-senti”, basi Bwana Chenge anazo nyingi zaidi alizoficha kushinda hizo! Kuna uwezekano Bwana Chenge anawajua “wenzake” walio na nyingi kuliko hizo alizo nazo katika benki ya nchi za nje!
Bwana Chenge ni m-Bunge wa Bariadi Masharik; ni m-Sukuma aliyejitetea, hapo baadaye, kwamba Kiswahili kinampiga chenga. Wengi hatukukubali kuwa Kiswahili kinampiga chenga, Chenge! Kuzunguka pote Tanzania kando ya Ziwa Victoria wazawa wanaelewa sana maana ya “vi-ji-senti”! Na wa-Tanzania wanajua matumizi ya Kiswahili ya vianzo vya “ki/vi”! Na wanaelewa sana wakati ambapo “ki” inapofuatiwa na “ji” kuwa “kiji…” au “viji…” katika muktadha wa kupunguza hadhi na thamani ya kizungumzwacho!
“Simply put”, uchu wa u-nyang’au wa baadhi ya walalaheri wa kufuatilia na kuchuma “vi-ji-senti” unaangamiza taifa letu, kama Johnson Mbwambo anavyowahi kuandika katika toleo la Raiamwema kuhusu “Ya Don Corleone, Yakuza na Mafisadi Wetu!
Je, TAKUKURU ilifanya kazi yake, kitaalamu? Haikufanikisha ushirikiano na Kamati Teule ya Bunge.
Je, yote yale Kamati Teule ya Bunge iliyoyagundua yalianikwa nje? Hapana!
Kwa nini Tanesco imegeuka kinyonga? Tanesco ilikataa kununua mitumba ya Dowans; Tanesco ikakubali na kukiuka msimamo wa Bodi yake; na sasa Tanesco imekataa tena!
Je, Tanesco sasa inasema, “Potelea mbali hata kama nchi inazama gizani?”
Je, Bodi ya Tanesco nayo ilifanya uamuzi mzuri wa kutaka kutuma tena wataalamu wa Tanesco waende huko Houston, Texas, kuzatiti bei hasa ya mitambo (turbines) hiyo ya kufua umeme? Ni kupoteza mapesa ya umma; Ofisi yetu ya u-Balozi, Washington, DC, inaweza kufanyakazi hiyo (kulingana na sera ya diplomasia ya uchumi).
Brela iliamua kuifuta “Richmond” ifikapo Septemba 15, 2008 kutokana na ufisadi na utata uliozalisha sakata la “Richmond”! Lakini kufuatia kushindwa kufua umeme wa dharura, leo hii bado tunaikumbatia “Richmond” kwa jina la “Dowans”! Malumbano yamejitokeza ya kukidhi mahitaji ya umeme kwa kununua mitumba ya mashini za “Richmond/Dowans”!
Wenye kutaka mitumba hiyo inunuliwe, wamezua mantiki ya kuunda na kutekeleza sera za umeme na nishati hadi 2014! Tunaihurumia “Dowans” na huruma hizo zimevalishwa nondo ya uzalendo, kwa upande wa Tanesco, Kamati ya Bunge uya Ununuzi – Mashirika ya Umma).
Waziri wa Madini na Nishati, na akili zake, kaamuru hiyo mitumba inunuliwe! Hata kwa Ikulu kidiriki kutamka eti Tanesco ni kampuni kamili yenye kufanya itakalo ni kukiuka uwajibikaji – uongozi unaokwenda kombo!
Kwa nini tusifikirie mbinu nyinginezo: nuklia (uranium tunayo kwa wingi..kwa nini wawekezaji wachimbe na kuuza nje kwa manufaa yao)! Jua tunalo, tena la masaa 12! Upepo tunao tena wa nguvu milimani, mabondeni na tambarare! Gesi tunayo tena inachotwa pengine kuuzwa nchi za nje! Maji-mvuke moto moto tunayo! Na vyanzo vinginevyo vya umeme na nishati tunavyo.
Kwa nini tunang’ang’ania mitambo mitumba, tena ya ghali, ya “Dowans” – kampuni ambayo haistahili kuwepo na Ambato imetushitaki huko Paris? Hivi tuliambiwa na Muumba kuwa chanzo cha umeme na nishati ni mabwawa yetu tu? Mbona hatujajifunza lolote (kama tunafundishika?) kuwa tunaathiriwa na ukame kila mwaka?
Lini tutaamka! Ama tuliishaga-kula “vi-ji-senti” vingi vya wawekezaji ambavyo vinatufunga nongwa na mitambo ya kufua umeme kwa mabawa ya maji? Si ni afadhali tufuge samaki kwa wingi katika mabwa hayo au tuyatumie katika umwagiliaji mashamba?
Nihitimishe na BAPism:
· Uchu wa u-nyang’au unaangamiza mataifa!
· Uchu wa u-nyang’au unaangamiza mfumo wa uchumi wa u-bepari wa Nchi za Magharibi!
· Uchu wa u-nyang’au unaangamiza nchi ya Tanzania kwa kutaka kuchuma ‘vi-ji-senti’!
· Uchu wa u-nyang’au hujikinga ki-sheria kwa kuvaa nondo ya “limited liability company” (LLC) au, kama tulivyozoea kuita, “limited” (Ltd), endapo kampuni itafikishwa mahakamani kwa ufisadi.
· Uchu wa u-nyang’au (kupitia baadhi ya “vigogo” na “wakubwa” na ma-wakala uchwara) hunyonya jasho la wananchi masikini wanaosamehewa madeni na nchi tajiri!

imeandikwa na MAggid Mjengwa

Saturday, March 28, 2009

World's first mass-produced electric car

While unveiling the sexy shape of its new Model S saloon, innovative US company, Tesla, announced that it would put the 'world's first mass-produced electric car' into production in 2011.

The Jaguar-esque shape and optimistic timeline are not the only reasons Tesla will be grabbing headlines around the world today (March 27), as claims to the Model S's abilities are quite staggering.

Utilising the company's advanced lithium-ion battery pack, the Model S sprints from 0-60mph in 'under six seconds' on the way to a top speed of 130mph. A Sport version will apparently cut the 0-60mph time by a further second.

Despite such performance, the Model S has been designed to carry up to seven occupants and masses of their luggage. That's thanks to a large space up front where the engine would normally reside, and a flat-floored interior with stowable seats.

The battery pack is located underneath the floor, which lowers the centre of gravity, as well as enhancing packaging. Tesla claims that it will be possible to swap the battery pack for a fully charged one in less time than it takes to fill a conventional car's fuel tank.

Even if battery-swapping facilities are not available, the Model S can be recharged from any 120-, 240- or 480V power supply, with an impressive 45-minute charge possible if the highest rating is available.

In ideal conditions, the Model S will have a range of 300-miles, though buyers will have to pay more for that capability, as the entry-level version does only 160-miles on a charge.

The 2011 launch is, however, dependant on Tesla receiving $350 million (about £242 million) in federal loans from the US government, which the company is confident it will receive.

Tesla will expand its dealer network outside the US with Munich and London earmarked for showrooms, possibly as early late 2009. Pricing is predicted to start at $49,900 in the US - about £34,500

source:http://uk.cars.yahoo.com/27032009/36/world-s-first-mass-produced-electric-car-0.html

Kp Leo
Kwaheri Professor Mukhululi
Head Priest Zekarias Gebre Michael of the Ethiopian Orthodox Church (centre) is accompanied by Ras Makonnen Tafari of the Priestly Order of Melchizedek (right) and one of his colleagues, as they prepare the coffin to receive the body of the late Professor Mkhululi, at his home in Njiro Hill, Arusha.
The Dean of the University of Dar es Salaam Business School (formerly the Faculty of Commerce and Management), Dr Marcellina Chijoriga, reads a speech on the work Professor Mkhululi did at the UDSM at his home in Njiro Hill.
The late professor’s daughter, Letsiwe Edwards, pays her last respects at the family home in Njiro Hill.
A section of hundreds of  mourners gather at the burial ground at Kijenge in Arusha

Professor Mkhululi laid to rest in Arusha 

Story and photos by IMAN MANI 
Professor Joshua Naphtali Mkhululi (formerly called Ken Edwards) was laid to rest in Kijenge, Arusha yesterday March 28, 2009. 

Hundreds of people from all walks of life paid their last  last respects  at his family home in Njiro Hill and  later on accompanied the casket to the burial grounds. 

Also  present was the Dean of the University of Dar es Salaam Business School (formerly the Faculty of Commerce and Management), Dr Marcellina Chijoriga. 

Dr. Chijoriga said that she could not miss such an opportunity to pay her respect to the person who was not only the first dean of the faculty but the brainchild behind its establishment.

On a more personal note in reference to the late Professor she added, “He was one of a special kind – putting everything in what he believed in.”

Being a member of the Rastafarian faith,  the  ceremony was conducted in accordance with the Ethiopian Orthodox Church’s principals, the the first time in Tanzania’s history for such proceedings. 

Head Priest Zekarias Gebre Michael, who came especially for this purpose from Nairobi, Kenya, the day before conducted the ceremony. 

Ras Makonnen Tafari of the Priestly Order of Melchizedek, based in Dar es Salaam, accompanied him together with two other colleagues. 

The late Professor Mkhululi, who died early this week in Dar es salaam,  has left behind six children and one grandchild. 

May Jah rest his soul in eternal peace

Amen



Unaposhangaa Ya Mussa....